Jarida la Mapishi

Supu ya kuku

Supu ya kuku | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 45
  • Walaji
    3

Supu ya kuku, ni supu tamu yenye viungo ambayo hupikwa kwa kuchemsha nyama ya kuku kwenye maji pamoja na viungo. Supu hii yafaa kula majira ya jioni kabla ya chakula cha jioni, katika kipindi cha msimu wa vuli. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya kuku.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa. Weka ndani ya hilo sufuria, kuku, maji, pilipili manga, chumvi, karafuu, majani ya mbei, mdalasini, vitunguu swaumu, iliki, tangawizi, pamoja na limao, halafu koroga vizuri, kisha weka sufuria hilo kwenye jiko lenye moto mkubwa, halafu acha ichemke.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria halafu acha iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 45, au hadi utakapo ona nyama ya kuku imeiva na kuwa laini.

    Step3

    Epua supu na upakue kwenye bakuli safi, tayari kwa kunywa.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.