Jarida la Mapishi

Supu ya nyanya na mboga

Supu ya nyanya na mboga | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 35
  • Walaji
    6

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kikaango kikubwa chenye mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hicho kikaango, jani la mbei, binzari nyembamba, pamoja na liki, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 3 mpaka 4, au hadi utakapo ona mashina ya liki zimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step2

    Weka vitunguu swaumu, tangawizi, pamoja na mashina ya figili, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2.

    Step3

    Weka mbegu za giligilani pamoja na mboga, kisha endelea kukaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 8 mpaka 10. Epua mchanganyiko huu na uweke kwenye kontena.

    Step4

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, nyanya pamoja na majani ya giligilani, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.

    Step5

    Ondoa mchanganyiko huo wa nyanya kutoka kwenye mashine ya kusaga na uweke kwenye kikaango ulichotumia kukaanga mboga. Weka chumvi pamoja na pilipili manga, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step6

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani. Weka maji, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 10.

    Step7

    Weka mchanganyiko wa mboga uliomo kwenye kontena na uchanganye vizuri, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 5 zaidi. Epua na upakue kwenye bakuli, tayari kwa kunywa.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.