Jarida la Mapishi

Supu ya tangawizi

Supu ya tangawizi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 30
  • Kupika
    Dakika 10
  • Walaji
    4

Supu ya tangawizi, ni supu tamu yenye harufu nzuri ya tangawizi. Kwa kawaida supu hii hupikwa kwa kutumia tangawizi, mbaazi, pamoja na viungo mbalimbali kama vile; binzari nyembamba na pilipili manga. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya tangawizi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua konten dogo. Weka ½ kikombe cha maji, kisha roweka mbaazi ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa dakika 30.

    Step2

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, mbaazi pamoja na maji uliyotumia kurowekea mbaazi, binzari nyembamba, pilipili manga, pamoja na tangawizi, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.

    Step3

    Chukua sufuria la ukubwa wa wastani. Weka kwenye hilo sufuria, mchanganyiko wa mbaazi ulio usaga, vikombe 4½ vya maji, pamoja na chumvi, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step4

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, halafu funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 5, kisha epua na umimine kwenye kontena. Funika vizuri kontena hilo, kisha weka pembeni.

    Step5

    Chukua sufuria dogo lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mbegu za haradali pamoja na majani ya mvuje, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30. Epua mchanganyiko huu na umimine kwenye kontena lenye supu, kisha changanya vizuri, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.