Jarida la Mapishi

Supu ya choroko

Supu ya choroko | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 30
  • Kupika
    Dakika 40
  • Walaji
    4

Supu ya choroko, ni supu tamu ambayo inasaidia sana katika kuboresha afya. Supu hii hupikwa kwa kitumia choroko, limao, pamoja na viungo vya aina mbalimbali kama vile; binzari ya manjano, binzari nyembamba na tangawizi. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya choroko.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka kikombe 1 cha maji, kisha roweka choroko ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa dakika 30.

    Step2

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria, choroko pamoja na maji uliyotumia kurowekea choroko, binzari ya manjano, chumvi, pamoja na vikombe 2 vya maji, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step3

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, halafu acha iendelee kuchemka huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 20 mpaka 30, au hadi utakapo ona choroko zimeiva, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.

    Step4

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka mchanganyiko wa choroko ulio chemsha kwenye hiyo mashine ya kusaga, kisha saga hadi utakapo ona choroko hizo zimesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huu kwenye mashine ya kusaga na urudishe kwenye sufuria.

    Step5

    Weka tangawizi kwenye mashine hiyo hiyo ya kusaga, kisha saga hadi utakapo ona tangawizi hiyo imesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa tangawizi kwenye mashine ya kusaga na uweke kwenye sufuria lenye mchanganyiko wa choroko.

    Step6

    Weka pia vikombe 4 vya maji vilivyobaki kwenye hilo sufuria, halafu koroga vizuri, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step7

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 5.

    Step8

    Chukua sufuria dogo lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mbegu za haradali, binzari nyembamba, pilipili manga, pamoja na majani ya mvuje, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30. Epua mchanganyiko huu na umimine kwenye sufuria lenye supu, kisha koroga vizuri.

    Step9

    Weka pia limao pamoja na majani ya giligilani halafu koroga tena vizuri, kisha acha ichemke.

    Step10

    Ukiona supu imechemka, epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Recipe Reviews

    • Ali Hamad

      Giligilani siijui na haradali sizijui

      • Mary Joachim

        Viungo vyote vilivyoandikwa humu vinapatikana kwenye masoko yote makubwa. Ukienda sokoni, nenda kaulizie kwenye maduka yanayouza viungo.

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.