![Vimanda vya viazi vya kuponda | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/10/vimanda_vya_viazi_vya_kuponda.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 25
-
Walaji4
Vimanda vya viazi vya kuponda, ni chakula kitamu ambacho hupikwa kwa kutumia viazi mviringo vilivyo chemshwa na kupondwa, mayai, vitunguu maji, pamoja na viungo. Chakula hiki chafaa kula kama kifungua kinywa wakati wa asubuhi, pamoja na kinywaji chochote ukipendacho. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika vimanda hivi vya viazi vya kuponda.
Ingredients
Directions
Chukua sufuria ndogo. Weka kwenye hilo sufuria kiazi mviringo pamoja na maji, kisha chemsha kwenye jiko lenye moto wa wastani kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona kimeiva.
Epua na umwage maji yote yaliyomo kwenye sufuria na kubakiwa na kiazi peke yake, kisha acha kipoe. Menya maganda ya viazi hivyo, kisha viponde vizuri.
Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka ndani ya hilo kontena, kiazi ulicho kiponda, mayai, vitunguu maji, ¼ kikombe cha majani ya giligilani, tangawizi, chumvi, pamoja na pilipili manga, kisha changanya vizuri.
Chukua kikaango kikubwa chenye mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hicho kikaango, mchanganyiko wa mayai uliochanganya, kisha funika kikaango na ukaange kwa muda wa dakika 3, au hadi utakapo ona upande wa chini wa mchanganyiko huo umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia. (Weka mchanganyiko huo kwa awamu 2 mpaka 3)
Nyunyizia ¼ kikombe cha majani ya giligilani yaliyobakia juu ya mchanganyiko huo wa mayai, kisha kandamiza taratibu majani hayo kwa kutumia kijiko cha kukaangia (spatula) ili yashikane vizuri na mchanganyiko huo wa mayai.
Telezesha kimanda kwenye sahani kubwa. Weka kijiko cha kukaangia juu ya kimanda na ukishikilie vizuri, kisha pindua sahani juu chini ili kimanda kipate kugeuka.
Rudisha kimanda kwenye sahani, kisha itelezeshe kwenye kikaango. Kaanga upande huo mwingine wa kimanda hicho kwa muda wa dakika 2, au hadi utakapo ona na upande huo umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Kunja kimanda hicho katikati, kisha epua na uweke kwenye sahani, tayari kwa kula.
Leave a Review