Jarida la Mapishi

Biskuti za shayiri na chocolate

Biskuti za shayiri na chocolate | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Saa 1
  • Kupika
    Dakika 15
  • Walaji
    30

Biskuti za shayiri na chocolate, ni biskuti tamu na laini, ambazo hupikwa kwa kutumia unga wa ngano, shayiri, pamoja na dark chocolate chips. Biskuti hizi zafaa sana kula kama kitafunio cha kawaida pamoja na glasi ya maziwa. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika biskuti hizi za shayiri na chocolate.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria ndogo. Weka siagi kwenye hilo sufuria, kisha weka sufuria hilo kwenye jiko lenye moto mkubwa, halafu acha siagi iyeyuke.

    Step2

    Chukua bakuli kubwa. Weka ndani ya hilo bakuli, siagi uliyo iyeyusha, pamoja na light brown sugar, kisha changanya vizuri.

    Step3

    Weka yai na vanilla extract, halafu endelea kuchanganya.

    Step4

    Weka shayiri, unga wa ngano, baking soda, chumvi, pamoja na dark chocolate chips, kisha changanya vizuri kwa kutumia mashine ya kuchanganyia (mixer), hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vyema na kuwa laini.

    Step5

    Chukua sinia la kuoka biskuti (cookie/biscuit sheet), na uweke ndani ya hilo sinia karatasi ya kuokea (baking paper). Weka vijiko vya mchanganyiko wa biskuti, kwenye hilo sinia la kuoka biskuti, hadi mchanyiko wote wa biskuti utakapo malizika.

    Step6

    Washa jiko la kuoka, na uweke joto la nyuzi 175° C, kisha acha jiko lipate moto. Jiko likishapata moto, weka sinia la kuoka biskuti ndani ya hilo jiko, na uoke kwa muda wa dakika 10 mpaka 15, au hadi utakapo ona biskuti zimeiva na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step7

    Biskuti zikisha iva, zitoe kwenye jiko la kuoka na uziweke pembeni ili zipoe kabla ya kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.