Jarida la Mapishi

Supu ya njegere

Supu ya njegere | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 45
  • Walaji
    4

Supu ya njegere, ni supu tamu yenye rangi ya kijani, ambayo yafaa kula katika msimu wa baridi. Supu hii hupikwa kwa kutumia njegere mbichi, mtindi, pamoja na viungo. Waweza kula supu hii pamoja na mkate au wali. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya njegere.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria la ukubwa wa wastani. Weka kwenye hilo sufuria, njegere pamoja na vikombe 2 vya maji, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, halafu funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona njegere zimeiva, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.

    Step3

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, njegere ulizo zichemsha pamoja na maji uliyotumia kuchemsha hizo njegere, kisha saga hadi utakapo ona njegere zimesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye kontena.

    Step4

    Weka kwenye hiyo hiyo mashine ya kusaga, mtindi, unga wa mahindi, pamoja na kikombe 1 cha maji, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vizuri. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye kontena jingine.

    Step5

    Weka kwenye hiyo hiyo mashine ya kusaga, vitunguu maji, tangawizi, pamoja na vitunguu swaumu, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.

    Step6

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka mchanganyiko wa vitunguu maji ulio usaga kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona mchanganyiko huo umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step7

    Weka mbegu za giligilani, binzari nyembamba, mchanganyiko wa njegere ulio usaga, chumvi, pamoja na vikombe 3 vya maji halafu koroga vizuri, kisha kisha weka moto mkubwa na uache ichemke.

    Step8

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 10.

    Step9

    Ongeza moto na uweke moto wa wastani. Mimina mchanganyiko wa mtindi ulio usaga na ukoroge vizuri, halafu acha ichemke kwa muda wa dakika 3, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.