Jarida la Mapishi

Supu ya nazi

Supu ya nazi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 30
  • Kupika
    Dakika 50
  • Walaji
    4

Supu ya nazi, ni supu nzuri ambayo hupikwa kwa kutumia tui la nazi pamoja na nazi iliyokunwa. Ukiachana na nazi, supu hii huwekewa viungo vya aina mbalimbali kama vile; binzari nyembamba, mbegu za haradali, n.k, ambavyo huifanya supu hii iwe tamu na yenye ladha ya kipekee zaidi. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya nazi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka vikombe 2 vya maji, kisha roweka mbaazi ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa dakika 30.

    Step2

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria, mbaazi pamoja na maji uliyotumia kurowekea mbaazi, binzari ya manjano, chumvi, pamoja na kikombe 1 cha maji, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step3

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, halafu acha iendelee kuchemka huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 30, au hadi utakapo ona mbaazi zimeiva, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.

    Step4

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka mchanganyiko wa mbaazi ulio chemsha kwenye hiyo mashine ya kusaga, kisha saga hadi utakapo ona mbaazi hizo zimesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huu kwenye mashine ya kusaga na urudishe kwenye sufuria.

    Step5

    Chukua sufuria jingine kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mbegu za haradali, binzari nyembamba, pilipili manga, majani ya mvuje, pamoja na nazi iliyokunwa, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step6

    Weka nyanya, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2.

    Step7

    Weka Tamarind Paste pamoja na vikombe 2 vya maji vilivyobaki, halafu koroga vizuri, kisha weka moto mkubwa na uache ichemke.

    Step8

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona nyanya zimeiva na kuwa laini.

    Step9

    Mimina mchanganyiko wa mbaazi ulio chemsha, halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 5.

    Step10

    Weka tui la nazi pamoja na majani ya giligilani halafu koroga vizuri, kisha acha iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 2 zaidi. Epua na upakue kwenye chombo safi tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.