Jarida la Mapishi

Supu ya maboga

Supu ya maboga | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 40
  • Walaji
    4

Supu ya maboga, nu supu tamu na rahisi kupika. Supu hii hupikwa kwa kutumia maboga, ambayo huchemshwa pamoja na viazi mviringo na viungo. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya maboga.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria, maboga, viazi mviringo, vitunguu maji, tangawizi, vitunguu swaumu, binzari ya manjano, chumvi, pamoja na vikombe 4 vya maji, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, halafu funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 30, au hadi utakapo ona maboga yameiva na kuwa laini, kisha epua supu na uweke pembeni ili ipoe.

    Step3

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka supu uliyo chemsha kwenye hiyo mashine ya kusaga, kisha saga hadi utakapo ona imesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa supu hiyo kutoka kwenye mashine ya kusaga na uirudishe kwenye sufuria.

    Step4

    Weka kwenye kwenye hilo sufuria limao pamoja na kikombe 1 cha maji yaliyobaki, harafu koroga vizuri, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa kwa muda wa dakika 2.

    Step5

    Chukua kikaango kidogo chenye mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hicho kikaango, black seeds, mbegu za uwatu, binzari nyembamba, pamoja na mbegu za shamari, halafu koroga vizuri. Epua na umimine mchanganyanyiko huu kwenye sufuria lenye supu, kisha koroga vizuri.

    Step6

    Acha supu iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 5 zaidi, kisha epua na upakue kwenye chombo safi tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.