-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 5
-
Walaji1
Garam masala, ni mchanganyiko wa viungo, ambao husiadia kuongeza ladha kwenye chakula. Garam masala yaweza kutumika kwenye chakula cha aina yoyote ile; kama vile supu, mchuzi, pilau, n.k. Neno “Garam” lina maana ya moto na Neno “Masala” lina maana ya viungo mchanganyiko. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kutengeza garam masala hii kwa ajili ya kuiuza, au kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
Ingredients
Directions
Chukua kikaango cha ukubwa wa wastani na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kikaango kipate moto. Weka kwenye hicho kikaango, mbegu za shamari, mbegu za binzari nyembamba, mbegu za pilipili manga, mbegu za iliki, pamoja na zafarani, halafu kaanga bila kutumia mafuta huku ukikoroga na kutikisa kikaango mara kwa mara kwa muda wa dakika 2, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.
Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga mchanganyiko ulio ukaanga, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye kontena.
Weka ndani ya hilo kontena, mdalasini, tangawizi, karafuu, basibasi, pamoja na kungumanga, kisha changanya vizuri.
Rudisha kikaango kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kikaango kipate moto. Weka mchanganyiko uliomo kwenye kontena kwenye hicho kikaango, halafu kaanga huku ukikoroga mara kwa mara, hadi utakapo ona mchanganyiko huo umepata moto, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.
Weka viungo hivyo kwenye chombo safi chenye mfuniko, kisha hifadhi mahali pakavu penye baridi.
Leave a Review