Jarida la Mapishi

Garam masala

Garam masala | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 5
  • Walaji
    1

Garam masala, ni mchanganyiko wa viungo ambao asili yake ni kutoka nchini India. Neno "Garam" lina maana ya moto na Neno "Masala" lina maana ya viungo mchanganyiko. Masala hii yafaa sana kutumika kwenye mchuzi au supu. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kutengeza garam masala hii kwa ajili ya kuiuza au kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kikaango cha ukubwa wa wastani na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kikaango kipate moto. Weka kwenye hicho kikaango, mbegu za shamari, mbegu za binzari nyembamba, mbegu za pilipili manga, mbegu za iliki, pamoja na zafarani, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2. Epua mchanganyiko huo na uweke pembeni ili upoe.

    Step2

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga mchanganyiko ulio ukaanga, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri. Ondoa mchanganyiko ulio usaga kutoka kwenye mashine ya kusaga, na uweke kwenye kontena safi.

    Step3

    Weka kwenye hilo kontena mdalasini, tangawizi, karafuu, basibasi, pamoja na kungumanga, kisha changanya vizuri.

    Step4

    Chukua mchanganyiko huo na urudishe kwenye kikaango, kisha kaanga tena kwenye jiko lenye moto wa wastani kwa muda wa dakika 2 zaidi. Epua mchanganyiko huo na uweke pembeni ili upoe.

    Step5

    Mchanganyiko huo ukishapoa, uhifadhi kwenye chombo chenye mfuniko na kutumia kidogo kidogo kwenye mapishi yako.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.