-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 1
-
Walaji1
Achari ya maembe mabichi, ni achari ya ambayo hutengenezwa kwa kutumia maembe mabichi, chumvi, sukari, pamoja na viungo vya aina mbali mbali. Achari hii yafaa kutumika kwenye chakula cha ina yoyote. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kutengeneza achari hii ya maembe mabichi.
Ingredients
Directions
Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, maembe, tangawizi, vitunguu vya kijani, majani ya mvuje, pamoja na chumvi, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.
Ondoa mchanganyiko huo kutoka kwenye mashine ya kusaga na uweke kwenye kontena. Weka sukari na ukoroge vizuri, kisha weka pembeni.
Chukua sufuria ndogo lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mbegu za haradali pamoja na mbegu za uwatu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30.
Epua mchanganyiko huo na umimine kwenye kontena lenye achari, kisha changanya vizuri, tayari kwa kutumia kwenye chakula cha aina yoyote ile.
Leave a Review