Jarida la Mapishi

Biriani ya kuku

Biriani ya kuku | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 30
  • Kupika
    Saa 1 Dk. 40
  • Walaji
    4

Biriani ya kuku, ni chakula kitamu ambacho hupikwa kwa kutumia mchele, nyama ya kuku, maziwa, mtindi, kaukau za vitunguu maji, nyanya, zafarani, pamoja na viungo vingine vingi. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika biriani hii ya kuku.

Bofya HAPA ili kujifunza jinsi ya kupika kaukau za vitunguu maji, ambazo utazitumia katika kupika biriani hii ya kuku.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, vitunguu swaumu, tangawizi, nyanya, pamoja na kikombe 1 cha majani ya giligilani, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye kontena kubwa.

    Step2

    Weka kwenye hilo kontena, mtindi, garam masala, pamoja na kijiko 1 cha chai cha chumvi, kisha koroga vizuri.

    Step3

    Weka nyama ya kuku, kisha changanya vizuri hadi utakapo ona vipande vyote vya nyama ya kuku vimeenea vyema viungo. Funika kontena hilo vizuri, kisha liweke kwenye friji kwa muda wa saa 8 mpaka saa 24.

    Step4

    Chukua kikombe chenye maziwa, kisha roweka zafarani ndani ya hicho kikombe chenye maziwa kwa muda wa dakika 30.

    Step5

    Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka maji, kisha roweka mchele ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa dakika 30.

    Step6

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria, mchele, maji uliyotumia kurowekea mchele, pamoja na ½ kijiko cha chai cha chumvi, halafu koroga vizuri, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step7

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, halafu acha iendelee kuchemka taratibu kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona maji kwenye sufuria yamekaribia kukauka na wali haujaiva, kisha epua na uweke pembeni. Hakikisha hukorogi kabisa wali wakati unaupika.

    Step8

    Mwaga maji yote yaliyomo kwenye sufuria na kubakiwa na wali peke yake.

    Step9

    Chukua sufuria jingine kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, iliki, mdalasini, majani ya mbei, binzari nyembamba, pamoja na mchanganyiko wa kuku ulio uweka kwenye friji halafu koroga vizuri, kisha zima jiko.

    Step10

    Weka kaukau za vitunguu maji, ½ kikombe cha majani ya giligilani, pamoja na majani ya minti juu ya huo mchanganyiko wa kuku, kisha sambaza vizuri.

    Step11

    Weka wali juu ya hivyo viungo, kisha sambaza vizuri.

    Step12

    Nyunyizia maziwa yenye zafarani juu ya huo wali.

    Step13

    Funika vizuri sufuria hilo kwa kutumia aluminium foil, kisha weka mfuniko juu ya hilo aluminium foil.

    Step14

    Washa jiko na uweke moto mkubwa, kisha pika biriani hiyo kwa muda wa dakika 10.

    Step15

    Punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha endelea kupika biriani hiyo kwa muda wa dakika 15.

    Step16

    Punguza moto tena na uweke moto mdogo, kisha endelea kupika biriani hiyo kwa muda wa saa 1, au hadi utakapo ona biriani imeiva.

    Step17

    Zima jiko, kisha changanya biriani hiyo vizuri, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.