Jarida la Mapishi

Pilau ya zafarani na lozi

Pilau ya zafarani na lozi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 30
  • Kupika
    Dakika 30
  • Walaji
    4

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka maji, kisha roweka mchele ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa dakika 30.

    Step2

    Chukua kikaango kidogo na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kipate moto. Weka njugu za pistachio kwenye hicho kikaango, halafu kaanga huku ukikoroga na kutikisa kikaango mara kwa mara kwa muda wa dakika 1, kisha epua na uweke pembeni.

    Step3

    Chukua bakuli ndogo. Weka maziwa, kisha roweka zafarani ndani ya hilo bakuli lenye maziwa kwa muda wa dakika 15.

    Step4

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, tangawizi, binzari nyembamba, iliki, pamoja na pilipili manga, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step5

    Weka mchele, maji uliyotumia kurowekea mchele, pamoja na chumvi, halafu koroga vizuri, kisha weka moto mkubwa na uache ichemke.

    Step6

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka taratibu kwa muda wa dakika 8 mpaka 10, au hadi utakapo ona wali umekaribia kuiva.

    Step7

    Funua sufuria na unyunyizie juu ya huo wali maziwa yenye zafarani, kisha funika tena sufuria na uendelee kupika huo wali kwa muda wa dakika 5 zaidi. Hakikisha hukorogi kabisa wali wakati unaupika.

    Step8

    Wali ukishaiva zima jiko na uache utulie kwa muda wa dakika 5, ukiwa bado juu ya jiko. Nyunyizia garam masala, lozi, pamoja na njugu za pistachio halafu koroga vizuri, kisha pakua pilau kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.