Jarida la Mapishi

Wali wa viazi

Wali wa viazi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 35
  • Walaji
    4

Wali wa viazi, ni chakula kitamu na rahisi sana kupika ambacho unaweza kukipika kwa muda mfupi sana wa ndani ya dakika 35 tu. Wali huu hupikwa kwa kutumia mchele, mtindi, nazi, viungo, pamoja na viazi mviringo vilivyo chemshwa. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika wali huu wa viazi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria dogo. Weka kwenye hilo sufuria viazi mviringo pamoja na maji, kisha chemsha kwenye jiko lenye moto wa wastani kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona vimeiva.

    Step2

    Epua na umwage maji yote yaliyomo kwenye sufuria na kubakiwa na viazi peke yake, kisha acha vipoe.

    Step3

    Menya maganda ya viazi hivyo, kisha vikate katika vipande vidogo vidogo.

    Step4

    Chukua kikaango kikubwa na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kikaango kipate moto. Weka nazi kwenye hicho kikaango, kisha kaanga bila kutumia mafuta huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1, au hadi utakapo ona imebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Weka tangawizi halafu endelea kukaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1 zaidi, kisha epua na uweke pembeni.

    Step6

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kiaha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba, mbegu za haradali, mbegu za uwatu, viazi mviringo, majani ya giligilani, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5.

    Step7

    Weka wali mweupe pamoja na mtindi halafu koroga vizuri, kisha funika sufuria na upike mchanganyiko huo kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona mtindi wote umekauka. Epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.