Jarida la Mapishi

Supu ya viazi

Supu ya viazi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 45
  • Walaji
    4

Supu ya viazi, ni supu tamu na rahisi kupika ambayo hupikwa kwa kutumia viazi mviringo, vitunguu maji, mtindi, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya viazi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria viazi mviringo pamoja na maji, kisha chemsha kwenye jiko lenye moto wa wastani kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona vimeiva.

    Step2

    Epua na umwage maji yote yaliyomo kwenye sufuria na kubakiwa na viazi peke yake, kisha acha vipoe.

    Step3

    Menya maganda ya viazi hivyo, kisha vikate katika vipande vidogo vidogo.

    Step4

    Chukua sufuria jingine kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mbegu za haradali pamoja na vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vitunguu vimeiva.

    Step5

    Weka tangawizi, majani ya mvuje, majani ya minti, pamoja na majani ya giligilani, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step6

    Weka mbegu za giligilani, kijiko 1 cha chai cha chumvi, pamoja na viazi ulivyo vichemsha, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 8 mpaka 10, au hadi utakapo ona viazi vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step7

    Mimina vikombe 2 vya maji halafu koroga vizuri, kisha weka moto mkubwa na uache ichemke.

    Step8

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, halafu funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona viazi vimeanza kumeguka, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.

    Step9

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, mchanganyiko wa viazi ulio upika, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini. Ondoa mchanganyiko huo kwenye mashine ya kusaga na uweke pembeni kwenye kontena.

    Step10

    Mimina mtindi ndani ya hilo kontena lenye supu halafu koroga vizuri, kisha funika vizuri kontena hilo na uliweke kwenye friji kwa muda wa saa 2 kabla ya kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.