Jarida la Mapishi

Supu ya maharage

Supu ya maharage | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 30
  • Kupika
    Dakika 50
  • Walaji
    4

Supu ya maharage, ni supu tamu na rahisi kupika. Supu hii hupikwa kwa kutumia maharage mekundu, mtindi, nyanya, tomato sauce, pamoja na viungo. Supu hii yafaa sana kunywa jioni pamoja na chakula chochote cha jioni. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya maharage.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria dogo. Weka kwenye hilo sufuria, maharage, maji, pamoja na chumvi, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, halafu funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 30, au hadi utakapo ona maharage yameiva, kisha epua na uweke pembeni.

    Step3

    Chukua sufuria la ukubwa wa wastani lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba pamoja na vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 3, au hadi utakapo ona vitunguu vimeiva.

    Step4

    Weka tangawizi, vitunguu swaumu, pamoja na nyanya, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, au hadi utakapo ona mchuzi umekuwa mzito.

    Step5

    Wela mbegu za giligilani pamoja na binzari ya manjano, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30.

    Step6

    Mimina mtindi taratibu huku ukikoroga, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 1.

    Step7

    Weka maharage uliyo chemsha, majani ya giligilani, pamoja na tomato sauce, halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 5.

    Step8

    Weka garam masala halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.