Jarida la Mapishi

Supu ya uyoga

Supu ya uyoga | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 15
  • Walaji
    4

Supu ya uyoga, ni supu tamu na yenye afya, ambayo hupikwa kwa kutumia uyoga mweupe au uyoga wa kahawia, mtindi, maziwa, pamoja na viungo. Upishi wa supu ya uyoga unahitaji sana uvumilivu ili uweze kupata ladha nzuri kwenye supu. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika supu hii ya uyoga.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kikaango kidogo na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kikaango kipate moto. Weka kwenye hicho kikaango, mbegu za pilipili manga pamoja na mbegu za binzari nyembamba halafu kaanga bila kutumia mafuta huku ukikoroga na kutikisa kikaango mara kwa mara kwa muda wa dakika 1, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.

    Step2

    Chukua kinu. Weka ndani ya hicho kinu, mbegu za pilipili manga pamoja na mbegu za binzari nyembamba ulizo zikaanga, kisha twanga hadi utakapo ona mbegu hizo zimesagika vizuri.

    Step3

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka liki kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona zimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step4

    Weka uyoga pamoja na vitunguu swaumu, halafu pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 7, au hadi utakapo ona uyoga umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.

    Step5

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, mchanganyiko wa uyoga ulio upika, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.

    Step6

    Chukua kontena kubwa. Weka ndani ya hilo kontena, mtindi, maziwa, mchanganyiko wa uyoga ulio usaga, limao, mchanganyiko wa pilipili manga ulio utwanga, pamoja chumvi, kisha koroga vizuri. Funika kontena hilo vizuri, kisha liweke kwenye friji kwa muda wa saa 2, kabla ya kula.

    Step7

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.