![Samaki wa kukaanga | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/11/samaki_wa_kukaanga.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 15
-
Walaji4
Samaki wa kukaanga, ni kitoweo kitamu na rahisi kupika, ambacho huandaliwa kwa kuchanganya samaki pamoja na viungo, kisha kukaanga kwenye mafuta. Kitoweo hiki cha samaki wa kukaanga, chafaa kula pamoja na wali mweupe, wali wa binzari nyembamba, wali wa nazi, au wali wa ukwaju. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika kitoweo hiki cha samaki wa kukaanga.
Ingredients
Directions
Chukua kontena kubwa. Weka ndani ya hilo kontena, pilipili manga, garam masala, mbegu za kisibiti, chumvi, tangawizi, vitunguu swaumu, pamoja na Tamarind Paste, kisha changanya vizuri.
Weka minofu ya samaki, kisha changanya vizuri hadi utakapo ona minofu yote ya samaki imeenea vyema viungo. Funika vizuri kontena hilo, kisha liweke kwenye friji kwa muda wa saa 1 mpaka saa 4.
Chukua kikaango kikubwa chenye vijiko 1½ vya chakula vya mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto mkubwa, kisha acha mafuta yapate moto kwa muda wa dakika 2. Weka vipande vya minofu ya samaki ndani ya hicho kikaango, kisha kaanga kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona upande huo wa chini wa minofu umebadilika rangi na kuwa na rangi kahawia.
Nyunyizia mafuta ya kupikia yaliyobaki juu ya hiyo minofu ya samaki. Geuza vipande hivyo vya minofu ya samaki, kisha endelea kukaanga kwa muda wa dakika 4, au hadi utakapo ona upande huo wa minofu ulio geuza umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Epua vipande hivyo vya minofu ya samaki na uviweke kwenye sahani. Nyunyizia limao juu ya hiyo minofu ya samaki, kisha weka mezani tayari kwa kula.
Leave a Review