Jarida la Mapishi

Saladi ya maharage

Saladi ya maharage | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Saa 1
  • Walaji
    4

Saladi ya maharage, ni saladi nzuri ambayo hutengenezwa kwa kutumia maharage mekundu, mtindi, ukwaju, majani ya minti, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Saladi hii yafaa kuliwa pamoja na nyama choma. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kutengeneza saladi hii ya maharage.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kikaango kidogo na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kikaango kipate moto. Weka mbegu za binzari nyembamba kwenye hicho kikaango, halafu kaanga bila kutumia mafuta huku ukikoroga na kutikisa kikaango mara kwa mara kwa muda wa dakika 1, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.

    Step2

    Chukua kinu. Weka ndani ya hicho kinu mbegu za binzari nyembamba ulizo zikaanga, kisha twanga hadi utakapo ona mbegu hizo zimesagika vizuri.

    Step3

    Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka vikombe 2 vya maji, kisha roweka maharage ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa saa 24.

    Step4

    Chukua sufuria la ukubwa wa wastani. Weka kwenye hilo sufuria, maharage, maji uliyotumia kurowekea maharage, vitunguu swaumu, iliki, mdalasini, pamojana chumvi, halafu koroga vizuri, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step5

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, halafu funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa saa 1, au hadi utakapo ona maji yamekauka na maharage yameiva, kisha epua na uweke pembeni kwenye kontena.

    Step6

    Chukua kontena jingine dogo. Weka ndani ya hilo kontena, mbegu za binzari nyembamba ulizo zitwangwa, mtindi, Tamarind Paste, tangawizi, pamoja na Chaat Masala, kisha koroga vizuri. Mimina mchanganyiko huu kwenye kontena lenye maharage, kisha changanya vizuri.

    Step7

    Weka majani ya giligilani pamoja na majani ya minti, kisha changanya tena vizuri, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.