Jarida la Mapishi

Pilau ya uwatu

Pilau ya uwatu | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 45
  • Walaji
    4

Pilau ya uwatu, ni chakula kitamu na rahisi kupika, ambacho hupikwa kwa kutumia mchele, viazi mviringo, majani mabichi ya uwatu, pamoja na viungo. Chakula hiki chafaa kula pamoja na kinywaji cha mtindi. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika pilau hii ya uwatu.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria ndogo. Weka maji kiasi, chumvi kiasi pamoja na kiazi, halafu chemsha kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona kiazi kimeiva, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe. Menya maganda yote ya hicho kiazi, kisha kikate katika vipande vidogo vidogo.

    Step2

    Chukua kikaango kikubwa chenye mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka majani ya uwatu kwenye hicho kikaango, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5.

    Step3

    Weka viazi, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, kisha endelea kukaanga mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona majani ya uwatu yamebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia. Epua mchanganyiko huo na uweke kwenye pilau ya binzari nyembamba.

    Step4

    Nyunyizia garam masala juu ya hiyo pilau, kisha changanya vizuri, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.