Jarida la Mapishi

Pilau ya tangawizi na minti

Pilau ya tangawizi na minti | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 30
  • Kupika
    Dakika 30
  • Walaji
    4

Pilau ya tangawizi na minti, ni chakula chenye ladha ya kipekee ambacho hupikwa kwa kutumia mchele, kitunguu maji, kiazi mviringo, tangawizi, pamoja na viungo vingine. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika pilau hii ya tangawizi na minti.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka maji, kisha roweka mchele ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa dakika 30.

    Step2

    Chukua kikaango kidogo na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kikaango kipate moto. Weka mbegu za binzari nyembamba kwenye hicho kikaango, halafu kaanga bila kutumia mafuta huku ukikoroga na kutikisa kikaango mara kwa mara kwa muda wa dakika 1, kisha epua na uweke pembeni ili ipoe.

    Step3

    Chukua kinu. Weka ndani ya hicho kinu mbegu za binzari nyembamba ulizo zikaanga, kisha twanga hadi utakapo ona mbegu hizo zimesagika vizuri.

    Step4

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu maji kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 7, au hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Weka viazi mviringo, tangawizi, pamoja na majani ya minti, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2.

    Step6

    Weka mchele, maji uliyotumia kurowekea mchele, pamoja na chumvi, halafu koroga vizuri, kisha weka moto mkubwa na uache ichemke.

    Step7

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka taratibu kwa muda wa dakika 10 mpaka 15, au hadi utakapo ona wali umeiva na maji yote kwenye sufuria yamekauka. Hakikisha hukorogi kabisa wali wakati unaupika.

    Step8

    Zima jiko, kisha acha pilau itulie kwa muda wa dakika 5, ikiwa bado juu ya jiko.

    Step9

    Nyunyizia binzari nyembamba uliyo ikaanga halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.