Jarida la Mapishi

Mishikaki ya nyama ya ng’ombe

Mishikaki ya nyama ya ng’ombe | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 10
  • Walaji
    4

Mishikaki ya nyama ya ng'ombe, ni mishikaki mitamu inayopikwa kwa kutumia nyama ya ng'ombe iliyokatwa vipande vipande vipande na kuchanganywa pamoja na viungo, kisha kuchomwa kwenye jiko la kuchomea nyama. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mishikaki hii ya nyama ya ng'ombe.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kontena dogo. Weka ndani ya hilo kontena, nyama ya ng'ombe, tangawizi, vitunguu swaumu, garam masala, pamoja na chumvi, kisha changanya vizuri hadi utakapo ona vipande vyote vya nyama ya ng'ombe vimeenea vyema viungo.

    Step2

    Funika kontena hilo vizuri, kisha liweke kwenye friji kwa muda wa saa 2.

    Step3

    Baada ya saa 2, ondoa kontena hilo kwenye friji na uliweke pembeni.

    Step4

    Chukua bakuli kubwa. Weka ndani ya hilo bakuli, mtindi, limao, nazi, pamoja na iliki, kisha changanya vizuri. Mimina mchanganyiko huu kwenye kontena lenye mchanganyiko wa nyama ya ng'ombe, kisha changanya vizuri hadi utakapo ona vipande vyote vya nyama ya ng'ombe vimeenea vyema mchanganyiko huu.

    Step5

    Funika kontena hilo vizuri, kisha liweke tena kwenye friji kwa muda wa saa 4.

    Step6

    Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka maji, kisha roweka vijiti vya mishikaki ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa dakika 30.

    Step7

    Baada ya dakika 30, mwaga maji yote yaliyomo kwenye kontena na kubakiwa na vijiti peke yake.

    Step8

    Chukua vijiti vya mishikaki, kisha chomeka vipande vya nyama ya ng'ombe kwenye hivyo vijiti.

    Step9

    Washa jiko la kuchomea nyama, kisha acha jiko lipate moto. Weka mishikaki juu ya jiko la kuchomea nyama, kisha choma mishikaki hiyo huku ukigeuza mara kwa mara kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona pande zote za mishikaki hiyo zimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step10

    Ondoa mishikaki hiyo kwenye jiko la kuchomea nyama na uiweke kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.