Jarida la Mapishi

Kuku wa kuoka

Kuku wa kuoka | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Saa 1
  • Walaji
    4

Kuku wa kuoka, ni pishi rahisi kupika ambalo nadhani mtu yoyote anayependa kupika anapaswa kulifahamu. Unachohitaji katika kupika pishi hili, ni viungo, chumvi pamoja na mafuta ya kupikia. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika kuku huyu wa kuoka.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua nyama ya kuku na uondoe ngozi yake yote.

    Step2

    Chukua kontena kubwa. Weka ndani ya hilo kontena, mtindi, mafuta ya kupikia, giligilani, vitunguu swaumu, tangawizi, pilipili manga, iliki, binzari nyembamba, mbegu za uwatu, pamoja na chumvi, kisha changanya hadi utakapo ona viungo vyote vimechanganyika vizuri.

    Step3

    Chukua nyama ya kuku na uiweke kwenye hilo kontena kubwa lenye viungo, kisha changanya vizuri, hadi utakapo ona upande wote wa nje na upande wa ndani ya tumbo la huyo kuku umechanganyika vyema na viungo. Funika vizuri kontena kwa kutumia mfuniko au plastic wrap, kisha weka kwenye friji kwa muda wa kati ya saa 2 hadi saa 24.

    Step4

    Washa jiko la kuoka na uweke joto la nyuzi 204° C, kisha acha jiko lipate moto. Chukua sinia la kuoka. Weka kuku juu ya hilo sinia, huku miguu ikiwa inatizama upande wa juu. Mimina juu ya kuku mchanganyiko wa viungo uliobaki kwenye kontena, halafu mpake vizuri kuku wote hivyo viungo ulivyomimina.

    Step5

    Nyunyizia juu ya huyo kuku, mdalasini, karafuu na majani ya minti, kisha funika nyama ya kuku kwa kutumia aluminium foil, halafu weka kwenye jiko la kuoka na uoke kwa muda wa dakika 40 au hadi utakapo oja upande wa juu wa kuku umeiva na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step6

    Baada ya dakika 40, fungua jiko la kuoka na utoe sinia la kuoka lenye kuku. Fungua aluminum foil, halafu geuza kuku juu chini, kisha funika tena kwa aluminium foil. Rudisha tena hiyo nyama ya kuku kwenye jiko la kuoka, kisha punguza moto na uweke joto la nyuzi 190° C. Eendelea kuoka kuku huyo kwa muda wa kati ya dakika 20 mpaka 30.

    Step7

    Kuku akisha iva, ondoa kutoka kwenye jiko la kuoka na umuweke pembeni kwa muda wa dakika 5, kabla ya kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Recipe Reviews

    • Minza ngaleha

      Joining instruction pls

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.