![Mchuzi wa nyama ya kusaga na viazi | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/11/mchuzi_wa_nyama_ya_kusaga_na_viazi.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 35
-
Walaji4
Ingredients
Directions
Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, iliki, mdalasini, majani ya mbei, binzari nyembamba, viazi, nyama ya kusaga, nyanya, majani ya giligilani, tangawizi, pamoja na vitunguu swaumu, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10.
Weka mbegu za giligilani, garam masala, mbegu za uwatu, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10 mpaka 15, au hadi utakapo ona nyama imebadilila rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Weka mtindi na ukoroge vizuri, kisha funika sufuria na uache ichemke kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona viazi vimeiva na mchuzi umekuwa mzito. Epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.
Conclusion
Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.
Leave a Review