-
Maandalizi-
-
KupikaSaa 1 Dk. 15
-
Walaji4
Ingredients
Directions
Chukua bakuli ndogo. Weka mtindi, kisha roweka zafarani ndani ya hilo bakuli lenye mtindi.
Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mdalasini, pilipili manga, iliki, majani ya mbei, karafuu pamoja na binzari nyembamba, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2.
Weka vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10 mpaka 12, au hadi utakapo ona vitunguu hivyo vimeiva.
Weka tangawizi, vitunguu swaumu, nyama, mbegu za giligilani, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona nyama imebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Weka maji na ukoroge vizuri, kisha acha ichemke katika moto mkubwa kwa muda wa dakika 5. Baada ya dakika 5, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 40, au hadi utakapo ona nyama imeiva.
Weka garam masala na ukoroge vizuri, halafu acha ichemke kwa muda wa dakika 5 zaidi, kisha epua na uweke pembeni.
Mimina mchanganyiko wa mtindi na zafarani kwenye hilo sufuria lenye nyama, kisha koroga vizuri, tayari kwa kula.
Conclusion
Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.
Leave a Review