![Mchuzi wa kamba | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/11/mchuzi_wa_kamba.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 40
-
Walaji4
Mchuzi wa kamba, ni kitoweo kitamu na rahisi kupika, ambacho hupikwa kwa kutumia kamba wabichi, nyanya, vitunguu maji, pamoja na viungo. Mchuzi huu wa kamba, wafaa kula pamoja na wali au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mchuzi huu wa kamba.
Ingredients
Directions
Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, vitunguu swaumu, tangawizi, majani ya mvuje, binzari nyembamba, mbegu za haradali, garam masala, chumvi, sukari, binzari ya manjano, pamoja na white vinegar, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri. Ondoa mchanganyiko huo kutoka kwenye mashine ya kusaga, na uweke pembeni kwenye kontena.
Weka nyanya kwenye hiyo hiyo mashine ya kusaga, kisha saga hadi utakapo ona nyanya hizo zimesagika vizuri na kuwa laini.
Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria mdalasini pamoja na majani ya mbei, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30.
Weka vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 7, au hadi utakapo ona vitunguu maji vimeiva.
Weka mchanganyiko ulio usaga, kisha pika mchanganyiko huo katika moto mdogo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona mchanganyiko huo umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Weka nyanya ulizo zisaga, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10, au hadi utakapo ona mchuzi umekuwa mzito.
Weka kamba kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 7, au hadi utakapo ona kamba wamebadilika rangi na kuwa na rangi ya pinki.
Weka majani ya giligilani na ukoroge vizuri, halafu acha ichemke kwa muda wa dakika 2, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.
Leave a Review