Jarida la Mapishi

Biskuti za chumvi na chocolate

Biskuti za chumvi na chocolate | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Saa 1 Dk. 15
  • Kupika
    Dakika 15
  • Walaji
    30

Biskuti za chumvi na chocolate, ni biskuti tamu na rahisi kupika zenye ladha ya chocolate yenye chumvi chumvi. Biskuti hizi zafaa kula kama kitafunio cha kawaida wakati wowote. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika biskuti hizi za chumvi na chocolate.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua bakuli kubwa. Weka ndani ya hilo bakuli, dark chocolate chips pamoja na sukari, kisha weka bakuli hilo ndani ya sufuria lenye maji ya moto, halafu acha viyeyuke. Ukiona vimesha yeyuka, weka mafuta ya nazi, kisha changanya vizuri.

    Step2

    Weka light brown sugar, dark brown sugar na mayai, halafu endelea kuchanganya.

    Step3

    Weka unga wa ngano, cocoa powder, chumvi, pamoja na baking powder, kisha changanya vizuri kwa kutumia, mashine ya kuchanganyia (mixer), hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vyema na kuwa laini.

    Step4

    Chukua sinia la kuoka biskuti (cookie/biscuit sheet), na uweke ndani ya hilo sinia karatasi ya kuokea (baking paper). Weka vijiko vya mchanganyiko wa biskuti, kwenye hilo sinia la kuoka biskuti, hadi mchanyiko wote wa biskuti utakapo malizika.

    Step5

    Washa jiko la kuoka, na uweke joto la nyuzi 175° C, kisha acha jiko lipate moto. Jiko likishapata moto, weka sinia la kuoka biskuti ndani ya hilo jiko, na uoke kwa muda wa dakika 15, au hadi utakapo ona biskuti zimeiva na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step6

    Biskuti zikisha iva, zitoe kwenye jiko la kuoka na uziweke pembeni ili zipoe kabla ya kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.