Jarida la Mapishi

Biriani ya mboga

Biriani ya mboga | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 30
  • Kupika
    Dakika 50
  • Walaji
    4

Biriani ya mboga, ni chakula kitamu na chenye harufu nzuri ambacho hupikwa kwa kutumia wali mweupe uliopikwa, maziwa, mboga mchanganyiko, mtindi, njugu mchanganyiko, pamoja na viungo. Biriani hii ya mboga kama zilizvyo biriani nyingine zote, ni chakula ambacho chafaa kuliwa kwenye sherehe au sikukuu. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika biriani hii ya mboga.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kikombe chenye maziwa, kisha roweka zafarani ndani ya hicho kikombe chenye maziwa kwa muda wa dakika 30.

    Step2

    Chukua kikaango kidogo na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kikaango kipate moto. Weka mchanganyiko wa njugu kwenye hicho kikaango, halafu kaanga bila kutumia mafuta huku ukikoroga na kutikisa kikaango mara kwa mara kwa muda wa dakika 3, au hadi utakapo ona zimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia, kisha epua na uweke pembeni.

    Step3

    Chukua sufuria kubwa lenye siagi na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha siagi iyeyuke. Weka kwenye hilo sufuria, mdalasini, karafuu, iliki, pamoja na majani ya mbei, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step4

    Weka vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 7, au hadi utakapo ona vitunguu maji vimeiva.

    Step5

    Weka tangawizi pamoja na vitunguu swaumu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step6

    Weka mchanganyiko wa mboga, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7.

    Step7

    Mimina mtindi taratibu huku ukikoroga, halafu acha ichemke kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona mtindi umekaribia kukauka, kisha epua na uweke pembeni.

    Step8

    Washa jiko la kuoka na uweke joto la nyuzi 175° C, kisha acha jiko lipate moto.

    Step9

    Chukua sufuria jingine kubwa. Mimina mchuzi wa mboga mchanganyiko uliyoipika kwenye hilo sufuria.

    Step10

    Weka nusu ya wali mweupe uliopikwa juu ya huo mchuzi, kisha sambaza vizuri.

    Step11

    Weka mchanganyiko wa mboga ulioupika juu ya huo wali, kisha sambaza vizuri.

    Step12

    Nyunzia limao, majani ya giligilani, pamoja na majani ya minti, juu ya huo mchanganyiko wa mboga.

    Step13

    Weka nusu ya wali uliobaki, kisha sambaza vizuri.

    Step14

    Nyunyizia maziwa yenye zafarani juu ya huo wali, kisha funika vizuri sufuria hilo kwa kutumia aluminium foil.

    Step15

    Weka sufuria hilo ndani ya jiko la kuoka, kisha oka kwa muda wa dakika 30, au hadi utakapo ona biriani imeiva. Ondoa sufuria hilo kwenye jiko la kuoka na uliweke pembeni.

    Step16

    Weka mchanganyiko wa njugu ulizo zikaanga kwenye hilo sufuria lenye biriani, kisha changanya vizuri, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.