![Wali wa viungo | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/11/wali_wa_viungo.jpg)
-
MaandaliziDakika 30
-
KupikaDakika 20
-
Walaji4
Ingredients
Directions
Chukua kontena la ukubwa wa wastani. Weka maji, kisha roweka mchele ndani ya hilo kontena lenye maji kwa muda wa dakika 30. Baada ya dakika 30, ondoa mchele kwenye hilo kontena na uweke kwenye chujio ili ujichuje maji.
Chukua sufuria la ukubwa wa wastani na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha lipate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba, pilipili manga, zafarani, pamoja na iliki, kisha kaanga huku ukikoroga na kutikisa sufuria mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.
Weka mchele, kisha endelea kukaanga huku ukiugeuza geuza mchele na kutikisa sufuria mara kwa mara, kwa muda wa dakika 2 mpaka 3 zaidi.
Weka maji uliyotumia kurowekea mchele pamoja na chumvi, halafu koroga vizuri, kisha weka moto mkubwa na uache ichemke.
Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka taratibu kwa muda wa dakika 10 mpaka 15, au hadi utakapo ona wali umeiva na maji yote kwenye sufuria yamekauka. Hakikisha hukorogi kabisa wali wakati unaupika.
Wali ukishaiva zima jiko na uache utulie kwa muda wa dakika 5, ukiwa bado juu ya jiko. Baada ya dakika 5, pakua pilau kwenye chombo safi, tayari kwa kula.
Leave a Review