Jarida la Mapishi

Wali wa mtindi

Wali wa mtindi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 20
  • Walaji
    4

Wali wa mtindi, ni chakula kikuu na maarufu sana ambacho hupikwa kwa kutumia wali uliochanganywa pamoja na mtindi na viungo. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika wali huu wa mtindi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria la ukubwa wa wastani. Weka kwenye hilo sufuria, mchele pamoja na maji, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, halafu funika sufuria na uache iendelee kuchemka taratibu kwa muda wa dakika 12 mpaka 15, au hadi utakapo ona wali umeiva na maji yote kwenye sufuria yamekauka, kisha epua na uweke pembeni. Hakikisha hukorogi kabisa wali wakati unaupika.

    Step3

    Chukua kikaango cha ukubwa wa wastani chenye mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hicho kikaango, vitunguu maji pamoja na tangawizi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step4

    Weka wali ulio upika pamoja na chumvi, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara, hadi utakapo ona wali umechanganyika vyema pamoja na vitunguu maji na tangawizi.

    Step5

    Weka mtindi pamoja na majani ya giligilani halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Conclusion

    Kabla ya kutumia mtindi huo, hakikisha unaupiga piga vizuri ukiwa kwenye bakuli kwa kutumia kijiko kama unavyo yapiga piga mayai unapotaka kuyakaanga, hadi utakapo ona mtindi umekuwa laini na hauna mabonge mabonge.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.