Jarida la Mapishi

Mchuzi wa mbaazi

Mchuzi wa mbaazi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 45
  • Walaji
    4

Mchuzi wa mbaazi, ni chakula kitamu, chenye virutubisho na rahisi kupika, ambacho chafaa kuliwa pamoja na wali, chapati au mkate. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mchuzi huu wa mbaazi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria, mbaazi, maji, chumvi, pamoja na binzari ya manjano, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 30 mpaka 40, au hadi utakapo ona mbaazi zimeiva.

    Step3

    Weka limao na ukoroge vizuri, halafu epua na uweke kwenye kontena, kisha funika vizuri kontena hilo.

    Step4

    Chukua sufuria dogo lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, vitunguu maji pamoja na majani ya mvuje, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2.

    Step5

    Weka binzari nyembamba, pamoja na tangawizi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step6

    Weka mbegu za giligilani, kisha endelea kukaanga kwa muda wa dakika 1 zaidi. Epua mchanganyiko huu na umimine kwenye kontena lenye mbaazi, kisha koroga vizuri, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.