Jarida la Mapishi

Bamia zenye vitunguu

Bamia zenye vitunguu | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 30
  • Walaji
    4

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kikaango kikubwa chenye mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha kikaango kipate moto. Weka bamia kwenye hicho kikaango, kisha kaanga bila kutumia mafuta huku ukizigeuza mara kwa mara kwa muda wa dakika 8 mpaka 10, au hadi utakapo ona bamia zimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia. Epua na uweke pembeni kwenye kontena.

    Step2

    Weka mafuta ya kupikia kwenye kikaango hicho hicho. Weka vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, au hadi utakapo ona vimeiva.

    Step3

    Weka bamia ulizo zikaanga mwanzoni, kisha kaanga huku ukizigeuza mara kwa mara kwa muda wa dakika 2 mpaka 3.

    Step4

    Weka mbegu za giligilani, binzari nyembamba, mango powder, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5.

    Step5

    Weka majani ya giligilani, kisha endelea kukaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 3 zaidi.

    Step6

    Nyunyizia garam masala na ukoroge vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.