Jarida la Mapishi

Mboga ya kabichi na choroko

Mboga ya kabichi na choroko | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 25
  • Walaji
    4

Mboga ya kabichi na choroko, ni mboga tamu, rahisi kupika na yenye afya, ambayo unaweza kuipika kwa muda mfupi sana wa ndani ya dakika 15 tu. Mboga hii hupikwa kwa kukaanga kabichi iliyo katwa katwa, choroko, pamoja na viungo. Unaweza kula mboga hii pamoja na wali au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mboga hii ya kabichi na choroko.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mbegu za haradali, mbegu za uwatu, mbegu za giligilani, majani ya mvuje, pamoja na tangawizi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2.

    Step2

    Weka kabichi, choroko, pamoja na chumvi, halafu koroga vizuri. Funika sufuria, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2 mpaka 3.

    Step3

    Punguza moto na uweke moto mdogo, kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 10 mpaka 15, au hadi utakapo ona choroko zimeiva.

    Step4

    Weka majani ya giligilani, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 zaidi.

    Step5

    Nyunyizia garam masala na ukoroge vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.