Jarida la Mapishi

Mchuzi wa mayai

Mchuzi wa mayai | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 45
  • Walaji
    4

Mchuzi wa mayai, ni chakula kitamu ambacho unaweza kukipika kwa muda mfupi wa ndani ya dakika 30 tu. Chakula hiki hupikwa kwa kutumia mayai yaliyo chemshwa, nyanya, pamoja na viungo. Unaweza kula chakula hiki pamoja na wali au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mchuzi huu wa mayai.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria la ukubwa wa wastani. Weka kwenye hilo sufuria maya 6 pamoja na maji kiasi, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 10 mpaka 12, au hadi utakapo ona mayai yameiva. Epua na uweke pembeni ili ipoe.

    Step3

    Menya maganda ya mayai hayo, kisha yakate katikati.

    Step4

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, nazi iliyokunwa, vitunguu swaumu, mbegu za giligilani, mbegu za haradali, binzari nyembamba, binzari ya manjano pamoja na star anise, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vyema na kuwa laini.

    Step5

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu maji kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vimeiva.

    Step6

    Weka mchanganyiko wa nazi ulio usaga, kisha endelea kukaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 zaidi.

    Step7

    Weka vikombe 3 vya maji, Tamarind Paste, pamoja na chumvi, halafu koroga vizuri,kisha weka moto mkubwa na uache ichemke.

    Step8

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 15, au hadi utakapo ona mchuzi umekuwa laini.

    Step9

    Mimina tui la nazi halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke.

    Step10

    Chukua kontena dogo. Weka ndani ya hilo kontena, vijiko vya chakula vya tui la nazi, pamoja na mayai yaliyobaki, kisha changanya kwa kupiga piga vizuri mchanganyiko huo.

    Step11

    Mimina mchanganyiko huo wa mayai kwenye sufuria lenye mchuzi, kisha koroga kwa muda wa dakika 2.

    Step12

    Weka mayai uliyo yachemsha, halafu acha ichemke kwa muda wa dakika 5, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.