![Mchuzi wa mayai | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/10/mchuzi_wa_mayai.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 45
-
Walaji4
Mchuzi wa mayai, ni chakula kitamu ambacho unaweza kukipika kwa muda mfupi wa ndani ya dakika 30 tu. Chakula hiki hupikwa kwa kutumia mayai yaliyo chemshwa, nyanya, pamoja na viungo. Unaweza kula chakula hiki pamoja na wali au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mchuzi huu wa mayai.
Ingredients
Directions
Chukua sufuria la ukubwa wa wastani. Weka kwenye hilo sufuria maya 6 pamoja na maji kiasi, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.
Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 10 mpaka 12, au hadi utakapo ona mayai yameiva. Epua na uweke pembeni ili ipoe.
Menya maganda ya mayai hayo, kisha yakate katikati.
Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, nazi iliyokunwa, vitunguu swaumu, mbegu za giligilani, mbegu za haradali, binzari nyembamba, binzari ya manjano pamoja na star anise, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vyema na kuwa laini.
Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu maji kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vimeiva.
Weka mchanganyiko wa nazi ulio usaga, kisha endelea kukaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 zaidi.
Weka vikombe 3 vya maji, Tamarind Paste, pamoja na chumvi, halafu koroga vizuri,kisha weka moto mkubwa na uache ichemke.
Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 15, au hadi utakapo ona mchuzi umekuwa laini.
Mimina tui la nazi halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke.
Chukua kontena dogo. Weka ndani ya hilo kontena, vijiko vya chakula vya tui la nazi, pamoja na mayai yaliyobaki, kisha changanya kwa kupiga piga vizuri mchanganyiko huo.
Mimina mchanganyiko huo wa mayai kwenye sufuria lenye mchuzi, kisha koroga kwa muda wa dakika 2.
Weka mayai uliyo yachemsha, halafu acha ichemke kwa muda wa dakika 5, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.
Leave a Review