Jarida la Mapishi

Mboga ya spinachi yenye viazi

Mboga ya spinachi yenye viazi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 40
  • Walaji
    4

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria, spinachi, viazi, maji, pamoja na chumvi, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 15 mpaka 20, au hadi utakapo ona viazi vimeiva.

    Step3

    Koroga mboga hizo kwa kasi ili kuvivunja baadhi ya viazi kwa ajili ya kupata mchuzi mzito kama krimu, kisha epua na uweke pembeni.

    Step4

    Chukua sufuria la ukubwa wa wastani lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba pamoja na vitunguu maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vitunguu maji vimeiva.

    Step5

    Weka tangawizi pamoja na vitunguu swaumu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara, hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step6

    Weka nyanya, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, au hadi utakapo ona mchuzi umekuwa mzito.

    Step7

    Weka mbegu za giligilani, garam masala, pamoja na binzari ya manjano, kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1 zaidi. Epua mchanganyiko huo na umimine kwenye sufuria lenye mchanganyiko wa spinachi, kisha changanya vizuri.

    Step8

    Funika sufuria hilo, halafu weka ichemke kwenye jiko lenye moto mdogo kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.