![Maboga ya kusaga yenye komamanga | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/10/maboga_ya_kusaga_yenye_komamanga.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 35
-
Walaji4
Maboga ya kusaga yenye komamanga, ni chakula ambacho hupikwa kwa kutumia maboga yaliyo sagwa, viungo, pamoja na mbegu za kokamanga zilizo kaushwa na kusagwa. Mbegu za komamanga ambazo huwekwa katika chakula hikiz husaidia kuongeza ladha na kukifanya chakula hiki kiwe kitamu zaidi. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika maboga haya ya kusaga yenye komamanga.
Ingredients
Directions
Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba, mbegu za uwatu, pamoja na mbegu za giligilani, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa sekunde 30.
Weka maboga, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 8 mpaka 10, au hadi utakapo ona maboga yamebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Punguza moto na uweke moto mdogo. Weka maji, kisha funika sufuria na uache ichemke huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona maboga yameiva na kuwa laini.
Weka sukari, mbegu za komamanga, pamoja na majani ya minti, halafu koroga vizuri, kisha funika tena sufuria. Epua na uweke pembeni itulie kwa muda wa dakika 30 mpaka 40, kabla ya kula.
Conclusion
Kumbuka kupasha moto maboga hayo, kabla ya kula.
Leave a Review