Jarida la Mapishi

Magimbi ya kuoka

Magimbi ya kuoka | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 50
  • Walaji
    4

Magimbi ya kuoka, ni chakula chenye ladha nzuri, ambacho hupikwa kwa kutumia magimbi yaliyo chemshwa, limao, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika magimbi haya ya kuoka.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria magimbi pamoja na maji, kisha chemsha kwenye jiko lenye moto wa wastani kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona yameiva.

    Step2

    Epua na umwage maji yote yaliyomo kwenye sufuria na kubakiwa na magimbi peke yake, kisha acha yapoe.

    Step3

    Menya maganda ya magimbi hayo, kisha yakate katika vipande vidogo vidogo.

    Step4

    Chukua sinia la kuokea. Weka kwenye hilo sinia, magimbi uliyo yachemsha, mafuta ya kupikia, limao, tangawizi, majani ya giligilani, mbegu za kisibiti, pamoja na chumvi, kisha changanya vizuri.

    Step5

    Washa jiko la kuoka na uweke joto la nyuzi 220° C, kisha acha jiko lipate moto. Weka sinia la kuokea lenye mchanganyiko wa magimbi ndani ya hilo jiko, kisha oka huku ukiyageuza magimbi mara kwa mara kwa muda wa dakika 20 mpaka 30, au hadi utakapo ona yamebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia. Ondoa magimbi hayo kwenye jiko la kuoka na uyaweke pembeni kwenye chombo safi.

    Step6

    Nyunyizia Chaat Masala, kisha changanya vizuri, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.