Jarida la Mapishi

Mchuzi wa bamia

Mchuzi wa bamia | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 35
  • Walaji
    4

Mchuzi wa bamia, ni mboga tamu inayopikwa kwa kutumia bamia mbichi, vitunguu, nyanya pamoja na viungo. Mboga hii yafaa kuliwa pamoja na ugali wali au hata chapati. Fiata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mchuzi huu wa bamia.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua kikaango kikubwa chenye vijiko 2 vya chai vya mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vipande vya bamia kwenye hicho kikaango, kisha kaanga huku ukivigeuza mara kwa mara kwa muda wa dakika 8 mpaka 10, au hadi utakapo ona pande zote za vipande hivyo vya bamia vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia. Epua na uweke pembeni, kisha ondoa vipande hivyo vya bamia kutoka kwenye kikaango, na uviweke pembeni kwenye kontena.

    Step2

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, tangawizi, vitunguu swaumu, nyanya, tui la nazi, Tamarind Paste, mbegu za giligilani, pamoja na binzari nyembamba, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.

    Step3

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia yaliyobaki na uliweke kwenye jiko lenye moto wa mkubwa, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye mchanganyiko ulio usaga kwenye hilo sufuria, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2 mpaka 3.

    Step4

    Punguza moto na uweke moto mdogo, kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, au hadi utakapo ona umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Weka binzari ya manjano, chumvi, pamoja na viazi mviringo, kisha endelea kupika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5.

    Step6

    Weka maji kiasi halafu koroga vizuri, kisha weka moto mkubwa na uache ichemke.

    Step7

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, au hadi utakapo ona viazi vimeiva na mchuzi umekuwa mzito.

    Step8

    Weka bamia ulizo zikaanga halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 5 zaidi.

    Step9

    Weka majani ya giligilani halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.