Jarida la Mapishi

Kachori

Kachori | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 35
  • Walaji
    4

Kachori, ni kitafunio kitamu ambacho hupikwa kwa kutumia mchanganyiko viazi mviringo vilivyo chemshwa, tomato sauce, white vinegar, pamoja na viungo ambavyo hufinyangwa katika umbo la mpira, kisha kukaangwa. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika kitafunio hiki cha kachori.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria kubwa. Weka kwenye hilo sufuria viazi mviringo pamoja na maji, kisha chemsha kwenye jiko lenye moto wa wastani kwa muda wa dakika 20, au hadi utakapo ona vimeiva.

    Step2

    Epua na umwage maji yote yaliyomo kwenye sufuria na kubakiwa na viazi peke yake, kisha acha vipoe.

    Step3

    Menya maganda ya viazi hivyo, halafu vikate katika vipande vidogo vidogo, kisha viponde vizuri.

    Step4

    Chukua kontena kubwa. Weka ndani ya hilo kontena, viazi ulivyo viponda pamoja na kijiko 1 cha chakula cha tangawizi, kisha changanya vizuri.

    Step5

    Chukua kiwango kidogo cha mchanganyiko wa viazi ulio changanya, halafu finyanga mchanganyiko huo kwa kutumia mikono yako ili kutengeneza umbo dogo la mpira, kisha weka pembeni kwenye sahani. Rudia hatua hii kwa mchanganyiko uliobaki, hadi utakapo ona mchanganyiko huo wote umemalizika na kupata mipira kati ya 20 hadi 25.

    Step6

    Chukua kikaango kikubwa chenye vijiko 2 vya chakula vya mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka mipira ya mchanganyiko wa viazi kwenye hicho kikaango, kisha kaanga huku ukivigeuza na kutikisa kikaango mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona pande zote za mipiria hiyo zimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia. Ondoa mipira hiyo ya viazi kwenye kikaango na uiweke pembeni kwenye kontena.

    Step7

    Weka kwenye kikaango hicho hicho kijiko 1 cha chakula cha mafuta ya kupikia yaliyobaki, kisha acha yapate moto. Weka ½ kijiko cha chakula cha tangawizi iliyobaki pamoja na vitunguu swaumu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step8

    Weka tomato sauce, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step9

    Weka white vinegar, sukari, pamoja na chumvi, kisha koroga vizuri.

    Step10

    Weka mipira ya viazi, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikitikisa kikaango mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona mpiria yote ya viazi imechanganyika vyema pamoja na mchanganyiko wa tomato sauce, pia hadi utakapo ona mchanganyiko wa tomato sauce umekaribia kukauka.

    Step11

    Weka vitunguu vya kijani, kisha pika mchanganyiko huo huku ukitikisa kikaango mara kwa mara kwa muda wa dakika 3 zaidi, kisha epua na uweke pembeni. Ondoa kachori hizo kwenye kikaango na uziweke kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.