![Curry powder | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/06/curry_powder.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 5
-
Walaji1
Curry powder, ni mchanganyiko wa viungo, ambayo asili yake ni kutoka nchini India. Curry powder husiadia kuongeza ladha kwenye chakula na waweza kuitumia kwenye chakula cha aina yoyote ile kama vile supu, mchuzi, saladi, n.k. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kutengeneza curry powder hii kwa ajili ya kuiza au kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
Ingredients
Directions
Chukua kikaango cha ukubwa wa wastani chenye mafuta ya kupikia na ukiweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu swaumu kwenye hicho kikaango, na ukaange kwa muda wa dakika 1, au hadi utakapo ona vitunguu swaumu vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Weka mbegu za shamari, mbegu za binzari nyembamba, mbegu za uwatu, mbegu za iliki, majani ya mbei pamoja na zafarani, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 2. Epua mchanganyiko huo na uweke pembeni ili upoe.
Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga mchanganyiko ulio ukaanga, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vizuri. Ondoa mchanganyiko ulio usaga kutoka kwenye mashine ya kusaga, na uweke kwenye kontena safi.
Weka kwenye hilo kontena, tangawizi, mdalasini, karafuu, basibasi, pamoja na kungumanga, kisha changanya vizuri.
Hifadhi mchanganyiko huo kwenye chombo chenye mfuniko na kutumia kidogo kidogo kwenye mapishi yako.
Leave a Review