Jarida la Mapishi

Biskuti za aprikoti na nazi

Biskuti za aprikoti na nazi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Saa 1 Dk. 15
  • Kupika
    Dakika 15
  • Walaji
    25

Biskuti za aprikoti na nazi, ni biskuti tamu, rahisi kupika na zenye ladha ya matunda halisi ya aprikoti pamoja na nazi. Biskuti hizi zafaa zaidi kuliwa kwenye sherehe. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika biskuti hizi za aprikoti na nazi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua bakuli kubwa. Weka ndani ya hilo bakuli, unga wa ngano, nazi, shayiri, matunda ya aprikoti, chumvi, pamoja na baking soda, kisha changanya vizuri.

    Step2

    Chukua bakuli nyingine ndogo. Weka ndani ya hiyo bakuli, siagi, light brown sugar, sukari na vanilla extract, halafu changanya vizuri.

    Step3

    Chukua mchanganyiko wa bakuli ndogo ya pili, na umimine kwenye mchanganyiko wa bakuli la kwanza. Weka dark chocolate chips, kwenye hilo bakuli la kwanza, kisha changanya vizuri kwa kutumia mashine ya kuchanganyia (mixer), hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vyema na kuwa laini.

    Step4

    Chukua sinia la kuoka biskuti (cookie/biscuit sheet), na uweke ndani ya hilo sinia karatasi ya kuokea (baking paper). Weka vijiko vya mchanganyiko wa biskuti, kwenye hilo sinia la kuoka biskuti, hadi mchanyiko wote wa biskuti utakapo malizika.

    Step5

    Washa jiko la kuoka, na uweke joto la nyuzi 175° C, kisha acha jiko lipate moto. Jiko likishapata moto, weka sinia la kuoka biskuti ndani ya hilo jiko, na uoke kwa muda wa dakika 10 mpaka 15, au hadi utakapo ona biskuti zimeiva na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step6

    Biskuti zikisha iva, zitoe kwenye jiko la kuoka na uziweke pembeni ili zipoe kabla ya kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.