![Mboga ya karoti na viazi | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/10/mboga_ya_karoti_na_nazi.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 20
-
Walaji4
Mboga ya karoti na viazi, ni mboga tamu na yenye afya ambayo hupikwa kwa kumia karoti, dengu, viungo, viazi mviringo, pamoja na tui la nazi. Waweza kula mboga hii kula pamoja na mlo wowote wa jioni, kama vile wali au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mboga hii ya karoti na nazi.
Ingredients
Directions
Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, mbegu za haradali, binzari nyembamba, dengu, mbegu za giligilani, chumvi, karoti, viazi mviringo, pamoja na maji, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 3 mpaka 4.
Punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na upike mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 15, au hadi utakapo ona viazi vimeiva na kuwa laini.
Nyunyizia limao pamoja na nazi halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.
Leave a Review