![Achari ya giligilani | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/11/achari_ya_giligilani.jpg)
-
Maandalizi-
-
Kupika-
-
Walaji1
Ingredients
Directions
Chukua sufuria ndogo lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria mbegu za haradali pamoja na mbaazi, kisha kaanga huku ukitikisa sufuria kwa muda wa dakika 1, au hadi utakapo ona mbaazi zimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia. Epua mchanganyiko huu na uweke pembeni ili upoe.
Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka mchanganyiko ulio ukaanga kwenye hiyo mashine ya kusaga, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.
Weka Tamarind Paste, chumvi, pamoja na majani ya giligilani, kisha endelea kusaga hadi utakapo ona mchanganyiko huo wote umesagika vyema na kuwa laini.
Ondoa mchanganyiko huo kutoka kwenye mashine ya kusaga, kisha uhifadhi kwenye chombo chenye mfuniko na kutumia kidogo kidogo kwenye chakula cha aina yoyote ile.
Leave a Review