Jarida la Mapishi

Muffins za machungwa na lozi

Muffins za machungwa na lozi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Saa 1 Dk. 5
  • Kupika
    Dakika 25
  • Walaji
    12

Muffins za machungwa na lozi, ni muffins ni tamu laini, ambazo hupikwa kwa kutumia, chungwa lililo kamuliwa, maganda ya chungwa yaliyo kunwa, pamoja na lozi zilizo katwa katwa. Muffins hizi zafaa kula kama kifungua kinywa wakati wa asubuhi. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika muffins hizi za machungwa na lozi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria ndogo. Weka ndani ya hilo sufuria maji ya kutosha pamoja na machungwa, kisha chemsha machungwa hayo kwa muda wa dakika 30, au hadi utakapo ona machungwa yamelainika. Epua na uweke pembeni ili yapoe.

    Step2

    Mwaga maji yote yaliyomo kwenye sufuria na kubakiwa na machungwa peke yake. Kata kata machungwa hayo katika vipande vidogo vidogo, kisha ondoa kokwa zote.

    Step3

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka machungwa kwenye hiyo mashine ya kusaga, kisha saga bila kuweka maji, hadi utakapo ona machungwa hayo yamesagika vyema na kuwa laini.

    Step4

    Chukua bakuli kubwa. Weka ndani ya hilo bakuli, mayai pamoja na sukari, kisha changanya vizuri.

    Step5

    Weka machungwa, unga wa lozi, baking powder, pamoja na chumvi, kisha changanya vizuri kwa kutumia, mashine ya kuchanganyia (mixer), hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vyema na kuwa laini.

    Step6

    Chukua sufuria la kuoka muffins (muffins pan), lenye matundu 12 ya muffins, na uweke ndani ya hayo matundu karatasi za kuokea muffin (muffin papers). Chukua bakuli lenye mchanganyiko ulio changanya na mashine ya kuchanganyia, na umimine mchanganyiko huo kwenye sufuria la kuoka muffins.

    Step7

    Washa jiko la kuoka, na uweke joto la nyuzi 175° C, kisha acha jiko lipate moto. Jiko likishapata moto, weka sufuria la kuoka muffins ndani ya hilo jiko, na uoke kwa muda wa dakika 20 mpaka 25, au hadi utakapo ona muffins zimeiva na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step8

    Muffins zikisha iva, ziondoe kwenye jiko la kuoka, kisha ziweke pembeni ili zipoe, zikiwa bado ndani ya sufuria la kuoka muffins. Muffins zikishapoa, unaweza kuzitoa ndani ya sufuria la kuoka muffins, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.