Jarida la Mapishi

Biringanya za nazi

Biringanya za nazi | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 45
  • Walaji
    4

Biringanya za nazi, ni mboga tamu iliyo sheheni ladha ya nazi, ambayo hupikwa kwa kutumia biringanya, nazi, kitunguu maji, majani ya minti, pamoja na viungo vya aina mbalimbali. Mboga hii yafaa sana kupika katika msimu wa kiangazi. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika biringanya hizi za nazi.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua mashine ya kusaga (blender). Weka kwenye hiyo mashine ya kusaga, nazi iliyokunwa, tangawizi, vitunguu swaumu, pamoja na vitunguu maji, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo umesagika vizuri na kuwa laini.

    Step2

    Weka mbegu za giligilani, garam masala, pamoja na binzari ya manjano, kisha saga hadi utakapo ona mchanganyiko huo wote umechanganyika vizuri.

    Step3

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka mchanganyiko wa nazi ulio usaga kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 3 mpaka 5, au hadi utakapo ona mchanganyiko huo umebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step4

    Weka biringanya, tui la nazi, pamoja na chumvi halafu koroga vizuri, kisha weka moto mkubwa na uache ichemke kwa muda wa dakika 4.

    Step5

    Punguza moto na uweke moto wa wastani, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 20 mpaka 30, au hadi utakapo ona biringanya zimeiva na kuwa laini.

    Step6

    Weka limao, majani ya giligilani, pamoja na majani ya minti halafu koroga vizuri, kisha acha ichemke kwa muda wa dakika 2 mpaka 4.

    Step7

    Nyunyizia garam masala halafu koroga vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.