![Mboga ya kauliflawa | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/11/mboga_ya_kauliflawa.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 40
-
Walaji4
Ingredients
Directions
Chukua sufuria kubwa lenye kijiko 1 cha chakula cha mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka viazi mviringo kwenye hilo sufuria, halafu kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vimebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia, kisha epua na uviweke pembeni kwenye kontena.
Weka kijiko 1 cha chakula cha mafuta ya kupikia kilicho bakia kwenye sufuria hilo hilo, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kauliflawa, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona imebadilika rangi na kuwa na rangi ya kahawia.
Punguza moto na uweke moto mdogo. Weka viazi mviringo ulivyo vikaanga mwanzoni, tangawizi, binzari ya manjano, pamoja na chumvi, halafu koroga vizuri, kisha funika sufuria, na upike mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 15 mpaka 25, au hadi utakapo ona kauliflawa na viazi vimeiva na kuwa laini.
Weka majani ya giligilani, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 zaidi.
Nyunyizia garam masala na ukoroge vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.
Leave a Review