![Mboga ya kauliflawa, karoti na maharage machanga | Jarida la Mapishi](https://www.jaridalamapishi.co.tz/wp-content/uploads/2023/11/mboga_ya_kauliflawa_karoti_na_maharage_machanga.jpg)
-
Maandalizi-
-
KupikaDakika 15
-
Walaji4
Mboga ya kauliflawa, karoti na maharage machanga, ni mboga tamu na rahisi kupika, ambayo unaweza kuipika kwa mfupi sana wa ndani ya dakika 30 tu. Mboga hii hupikwa kwa kutumia kauliflawa, karoti, maharage machanga, vitunguu maji, pamoja na viungo. Mboga hii yafaa sana kula pamoja na wali wa binzari ya manjano, au chapati. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika mboga hii ya kauliflawa.
Ingredients
Directions
Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka kwenye hilo sufuria, binzari nyembamba, mbegu za kisibiti, vitunguu maji pamoja na tangawizi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.
Weka vitunguu swaumu, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.
Weka mbegu za giligilani, binzari ya manjano, vikombe vya mboga mchanganyiko, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5.
Weka nyanya, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.
Funika sufuria vizuri, kisha pika mboga hizo kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona zimeiva.
Weka white vinegar pamoja na majani ya giligilani, kisha endelea kupika mboga hizo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1 zaidi.
Nyunyizia garam masala na ukoroge vizuri, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.
Leave a Review