Jarida la Mapishi

Chai ya shamari na iliki

Chai ya shamari na iliki | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Dakika 5
  • Walaji
    2

Chai ya shamari na iliki, ni chai nzuri sana ambayo inasaidia mtu ambaye amevimbiwa na tumbo la chakula. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kutengeneza chai hii ya shamari na iliki.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua sufuria la ukubwa wa wastani. Weka kwenye hilo sufuria, maji, iliki, pamoja na mbegu za shamari, kisha weka ichemke kwenye jiko lenye moto mkubwa.

    Step2

    Ukiona imeanza kuchemka, punguza moto na uweke moto mdogo, kisha funika sufuria na uache iendelee kuchemka taratibu, hadi utakapo ona maji yamebadilika rangi na kupungua kwa kiwango cha ⅓.

    Step3

    Weka majani ya chai halafu koroga vizuri, kisha zima jiko na uache chai itulie kwa muda wa dakika 2.

    Step4

    Mimina maziwa halafu koroga vizuri, kisha washa tena jiko na uache ichemke.

    Step5

    Ukiona imechemka, zima jiko, kisha epua na uweke pembeni.

    Step6

    Chukua vikombe 2 pamoja na chujio. Chuja chai ndani ya hivyo vikombe. Weka sukari kadiri ya mahitaji yako, kisha koroga vizuri, tayari kwa kunywa.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.