Jarida la Mapishi

Biringanya za kuponda zenye njegere

Biringanya za kuponda zenye njegere | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    -
  • Kupika
    Saa 1 Dk. 10
  • Walaji
    4

Ingredients

    Directions

    Step1

    Washa jiko la kuoka (oven) na uweke joto la nyuzi 205° C, kisha acha jiko lipate moto. Chukua mafuta ya kupikia na upake kwenye ngozi ya nje ya biringanya, kisha chukua kisu na uchanje sehemu mbali mbali za biringanya hizo kwa kutumia ncha ya kisu.

    Step2

    Weka biringanya ndani ya jiko la kuoka, kisha oka kwa muda wa dakika 30 mpaka 40, au hadi utakapo ona biringanya hizo zimekuwa laini. Ondoa biringanya hizo kutoka kwenye jiko la kuoka na uziweke pembeni ili zipoe.

    Step3

    Menya maganda ya biringanya hizo halafu ziponde vizuri, kisha ziweke kwenye kontena.

    Step4

    Chukua sufuria kubwa lenye mafuta ya kupikia na uliweke kwenye jiko lenye moto wa wastani, kisha acha mafuta yapate moto. Weka vitunguu maji kwenye hilo sufuria, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5, au hadi utakapo ona vitunguu vimeiva.

    Step5

    Weka vitunguu swaumu, mbegu za giligilani, binzari nyembamba, garam masala, pamoja na chumvi, kisha kaanga huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 1.

    Step6

    Weka nyanya pamoja na majani ya giligilani, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 5 mpaka 7, au hadi utakapo ona mchuzi wa nyanya umekuwa mzito.

    Step7

    Punguza moto na uweke moto mdogo. Weka biringanya ulizo ziponda pamoja na njegere, kisha pika mchanganyiko huo huku ukikoroga mara kwa mara kwa muda wa dakika 15.

    Step8

    Mimina cream huku ukikoroga, halafu acha ichemke kwa muda wa dakika 1, kisha epua na upakue kwenye chombo safi, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.