Jarida la Mapishi

Muffins za mdalasini na matunda damu

Muffins za mdalasini na matunda damu | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 35
  • Kupika
    Dakika 25
  • Walaji
    12

Muffins za mdalasini na matunda damu, ni muffins tamu ambazo zenye ladha ya mchanganyiko wa mdalasini pamoja na matunda damu yaliyo katwa katwa na kuondolewa kokwa. Muffins hizi zafaa sana kuliwa katika kipindi cha msimu wa vuli. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika muffins hizi za mdalasini na matunda damu.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua bakuli kubwa. Weka ndani ya hilo bakuli, unga wa ngano, light brown sugar, baking soda, mdalasini, tangawizi pamoja na jozi, kisha changanya vizuri.

    Step2

    Weka buttermilk, mafuta ya kupikia, yai, vanilla extract, pamoja na matunda damu, kisha changanya vizuri kwa kutumia mashine ya kuchanganyia (mixer), hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vyema na kuwa laini.

    Step3

    Chukua sufuria la kuoka muffins (muffins pan), lenye matundu 12 ya muffins, na uweke ndani ya hayo matundu karatasi za kuokea muffin (muffin papers). Chukua bakuli lenye mchanganyiko ulio changanya na mashine ya kuchanganyia, na umimine mchanganyiko huo kwenye sufuria la kuoka muffins.

    Step4

    Washa jiko la kuoka, na uweke joto la nyuzi 175° C, kisha acha jiko lipate moto. Jiko likishapata moto, weka sufuria la kuoka muffins ndani ya hilo jiko, na uoke kwa muda wa dakika 20 mpaka 25, au hadi utakapo ona muffins zimeiva na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Muffins zikisha iva, ziondoe kwenye jiko la kuoka, kisha ziweke pembeni ili zipoe, zikiwa bado ndani ya sufuria la kuoka muffins. Muffins zikishapoa, unaweza kuzitoa ndani ya sufuria la kuoka muffins, tayari kwa kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.